Amorim afikia 'level' za Ferguson na Busby Man United
Sisti Herman
December 13, 2024
Share :
Baada ya kuisaidia klabu yake kushinda 2-1 dhidi ya Viktoria Plzen, Ruben Amorim ameingia kwenyerekodi ya kuwa kocha wa tatu wa Manchester United kushinda mechi 3 mfululizo za kwanza michuano ya Ulaya akiungana na Sir Alex Ferguson na Sir Matt Busby.
Amorim ameshinda michezo yake mitatu ya mwanzo ya UEFA Europa League ambayo ni;
- PAOK Thesaloniki, 2-0
- Bodo/Glimt, 3-2
- Viktora Plzen, 2-1
Kwenye mchezo wa jana Man Utd imeshinda kwa magoli ya kipindi cha pili ya nyota wa Denmark Rasmus Hojlund ambaye alianzia benchi na kuingia kipindi cha pili.