pmbet

Bi harusi afariki kwenye sherehe yake akimuimbia mume wake.

Joyce Shedrack

October 28, 2024
Share :

Sherehe ya harusi iliyofanyika siku ya jumamosi octoba 26 Nchini Cameroon imegeuka kuwa vilio na huzuni  baada ya bi harusi anayejulikana kama Sorelle Manuella kuanguka akiwa anaimba na kucheza wimbo maalum kwa ajili ya mumewe. 

 

Bi harusi huyo aliyefariki kutokana na mshtuko wa moyo kwa mujibu wa ripoti za madaktari hapo awali watu wengi walidhani kuanguka kwake ilikuwa ni sehemu ya onyesho lake kabla ya watu kugundua na juhudi za kumpa huduma ya kwanza zikagonga mwamba. 

 

Muda mfupi baada ya kupelekwa  hospitali  madaktari walitangaza na kuthibitisha kuwa mwanamama huyo tayari amefariki.

 

Sorelle ameacha mume ambaye alifunga naye ndoa muda mfupi kabla ya kifo chake na binti watatu wachanga, mdogo zaidi akiwa na umri   chini ya mwaka mmoja.

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet