Camara amkimbiza Diarra kwa Clean Sheets Ligi Kuu
Sisti Herman
February 3, 2025
Share :
Ile vita ya kuwani tuzo ya kipa bora wa msimu wa Ligi kuu Tanzania bara ni kama imemsogelea zaidi kipa wa klabu ya Simba Moussa Camara zaidi ya kipa wa klabu ya Yanga Djigui Diarra kutokana na utofauti wa takwimu baina yao hadi sasa msimu huu.
Hadi sasa kwenye Ligi kuu Camara anaongoza kwa idadi ya hati safi (Clean Sheets) baada ya kucheza michezo 16 na kutoruhusu kufungwa goli kwenye michezo 13, sawa na wastani wa 0.81 wa idadi ya mechi na Clean Sheets.
Kwa upande wa Diarra hadi sasa kwenye Ligi kuu amecheza mechi 10 na kutoruhusu kufungwa goli kwenye mechi 8, sawa na wastani wa 0.8 wa idadi ya mechi na Clean Sheets.