Ibrahim Kone aandika ujumbe mzito baada ya kuvunjika mguu uwanjani.
Joyce Shedrack
June 20, 2026
Share :
Mchezaji wa Ismaël Koné amezungumza kwa mara ya kwanza tangu apate jeraha baya la kuvunjika mguu, kwenye mchezo dhidi timu ya taifa ya Indonesia jeraha ambalo litamfanya kukaa nje ya uwanja kwa miezi 5-6.
"ALLAH hajawahi kuniangusha.Katika maisha yangu yote, hata mara moja.
Kwa hiyo kwa nini nimtilie shaka sasa? Hasa nikijua kwamba Yeye anajua na kuona kila kitu kabla hata hakijatokea.
Ana mpango na maono kwa kila mmoja wetu.Mapambano haya ni mtihani wa imani yangu Kwake na wa tabia yangu.
Na kwa kweli niko tayari kwa hilo, kwa sababu ALLAH hatakupa changamoto ambayo huwezi kuishinda. Na kujaribiwa ni mojawapo ya zawadi kubwa kutoka kwa Mungu.Upendo na msaada wenu nimeuhisi kwa dhati. Asanteni sana.
Hamwezi hata kufikiria jinsi ninavyoshukuru kila mmoja aliyenifikia na kunikumbuka katika dua na maombi yake.
Ninamshukuru Mungu kwa hilo, kwa sababu si kila mtu ana bahati ya kupata jambo kama hili.
Kwa ndugu zangu wa Canada, nilipojigeuza kuwa kocha msaidizi ili kuwaunga mkono kutoka pembeni ya uwanja 😂, nilitaka mjue kwamba ninawapenda kutoka moyoni kabisa, na undugu wetu una maana kubwa sana kwangu.
Kile mlichokifanya jana kitabaki moyoni mwangu milele,Nitarejea hivi karibuni, na tutaendelea kutengeneza kumbukumbu nyingi zaidi pamoja"Ameandika Kone.





