pmbet

Man United na Spurs kuumana leo fainali ya Europa League

Sisti Herman

May 21, 2025
Share :

Fainali ya UEFA Europa League leo, Mei 21, 2025, itawashirikisha Tottenham Hotspur dhidi ya Manchester United kwenye Uwanja wa San Mamés huko Bilbao, Hispania. Mechi itaanza saa 8:00 PM (saa za Uingereza) au saa 4:00 AM (saa za Afrika Mashariki, Mei 22, 2025).
 


Dondoo muhimu kuelekea mchezo huu.

Manchester United: Wao ndio timu pekee ambayo haijapoteza mchezo katika mashindano makubwa ya Ulaya msimu huu, wakiwa na ushindi 9 na sare 5 katika mechi 14 za Europa League.

- Wamefunga magoli 35, idadi ya pili kwa juu katika historia ya UEFA Cup/Europa League.

- Bruno Fernandes ameongoza kwa magoli 7 na asisti 4, huku Mason Mount, Casemiro, na Rasmus Højlund wakiwa wachezaji muhimu.

- Kocha Ruben Amorim anaweza kuwa kocha wa tatu kushinda taji kubwa katika msimu wake wa kwanza na United.

- Leny Yoro, Diogo Dalot, na Joshua Zirkzee wamerudi mazoezini, lakini Lisandro Martinez na Matthijs de Ligt wako nje kwa majeraha.


Tottenham Hotspur: Wanatafuta taji lao la kwanza la kimataifa tangu UEFA Cup ya 1983-84 na taji lao la kwanza la Ligi tangu 2007-08. Wameshinda mechi 9 kati ya 14 za Europa League msimu huu, rekodi yao bora zaidi.

- Dominic Solanke amefunga mabao 5 dhidi ya United katika mechi zake nne za mwisho.

- Hata hivyo, wanakosa wachezaji muhimu kama Dejan Kulusevski (kwa jeraha la goti), James Maddison, Lucas Bergvall, na Radu Dragusin (asiyestahiki).

- Kocha Ange Postecoglou ni kocha wa kwanza wa Australia kufikisha timu kwenye fainali ya Ulaya.

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet