pmbet

Mtuhumiwa mauaji ya Tupac Shakur anyimwa dhamana.

Joyce Shedrack

August 31, 2024
Share :

Jaji wa Mahakama ya Wilaya ya Clark Nchini Marekani Carli Kierny amemnyima tena dhamana mtuhumiwa wa maujai ya mwanamuziki Tupac Shakur, Duane “Keffe D” Davis  mauaji yaliyotokea mwaka 1996 Jijini Los Angeles.

Keffe D ambaye mara kwa mara amekuwa akiomba dhamana ameomba dhamana kwa mara nyingine ili aweze kwenda kupatiwa matibabu lakini mahakama hiyo imemkatalia dhamana  toka alivyokamatwa kwa mara ya kwanza  mwaka 2023.

Kierny ambaye ni jaji wa mahakama hiyo ameweka wazi sababu ya kutokupokea dhamana hiyo ni kutokana na kuwa na hisia mbaya zinazojaribu kufichwa na mtoaji wa dhamana hiyo ambaye ni "Wack 100".

Keffe D amekana mashtaka ya mauaji ya daraja la kwanza na kesi hiyo imesogezwa mbele kutoka Novemba 4, 2024 hadi Machi 17 mwakani itakaporindima tena.

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet