P Diddy kumuajiri Mwanasheria wa Young Thug .
Joyce Shedrack
April 17, 2025
Share :
Rapa maarufu wa Marekani anayeshikiliwa na polisi P Diddy yupo kwenye mpango wa kuimarisha safu yake ya mawakili ambao watampambania kwenye kesi zinazomkabili zinazotarajiwa kusikilizwa kuanzia Mei 5 mwaka huu.
Taarifa kutoka kwenye vyombo mbalimbali vya habari vinaripoti kuwa Diddy amepanga kumuongeza wakili maarufu ambaye alimtetea rapa Young Thug kwenye mashataka yake ya YSL RICO, Georgia Brian Steel.
Timu ya mawikili ya rapa huyo imekuwa ikifanya jitahada kubwa za kumnasua kwenye sakata la kisheria linalomkabili tangu mwaka 2024 na kesi nyingine mpya zilizoibuka hivi karibuni.