pmbet

Treni zagongana na kusababisha kifo cha dereva na kujeruhi 89

Eric Buyanza

June 20, 2026
Share :

Dereva wa treni amefariki dunia na watu 89 kujeruhiwa baada ya treni mbili kugongana katika eneo la Bedford nchini Uingereza.

 

Watu 11 walipata majeraha mabaya sana, 22 walijeruhiwa vibaya, na wengine 56 walipata majeraha madogo.
 

Ajali hiyo ilihusisha treni mbili za kampuni ya East Midlands Railway (EMR) zilizokuwa zikielekea kusini kwenda London St Pancras siku ya Ijumaa alasiri. Chanzo cha ajali hiyo bado kinachunguzwa.

 

Katibu Mkuu wa chama cha wafanyakazi wa reli cha RMT, Eddie Dempsey, alisema chama hicho “kimehuzunishwa sana kusikia kwamba dereva wa treni na aliyekuwa mwakilishi wa RMT amefariki katika ajali hiyo.”
 

Katika taarifa yake, Polisi wa Usafiri wa Uingereza (BTP) walisema wametangaza tukio hilo kuwa dharura kubwa baada ya mgongano huo uliotokea saa 11:15 jioni kwa saa za Uingereza.

 

“Tunaelewa kuwa watu kadhaa wamejeruhiwa na kwa masikitiko makubwa mtu mmoja amefariki dunia,” taarifa hiyo ilisema.

 

Huduma za treni za East Midlands Railway kwenda na kutoka London St Pancras zilisimamishwa kwa muda wote wa Ijumaa jioni, na usumbufu wa safari unatarajiwa kuendelea hadi Jumamosi.

 

Mmoja wa abiria, Dkt. Peter Knapp, aliiambia BBC kwamba alikuwa akisafiri katika behewa la mbele la treni iliyogongana na nyingine.

 

“Niliposimama, niliona viti vimetapakaa kila mahali. Ilikuwa ni kana kwamba nilikuwa kwenye mlipuko wa bomu.

 

“Niliposimama, niliona nyuso za watu zikiwa zimejaa damu, baadhi ya miguu yao ilionekana kuvunjika, na moshi ulikuwa kila mahali,” alisema.
 

BBC

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet