Ulaya na Marekani hawafanyi vizuri kiuchumi kama Tanzania.
Joyce Shedrack
June 16, 2025
Share :
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, amewahimiza Watanzania kujenga uchumi wa ndani kwa kuacha kutegemea misaada kutoka nje, akisisitiza kuwa hali ya dunia kwa sasa si ya kutegemewa kutokana na changamoto mbalimbali za kiuchumi na kijamii.
Akizungumza na wananchi wa mkoa wa Simiyu katika ziara yake ya kikazi leo tarehe 16 Juni 2025, Rais Samia amesema kuwa Tanzania inaendelea kufanya vizuri kiuchumi licha ya hali ngumu inayozikumba nchi nyingi duniani, zikiwemo zile zilizoendelea na hata baadhi ya mataifa ya Afrika Mashariki.
“Ukitegemea msaada wale wanaotoa msaada dunia yote sasa ipo juu chini. Mavita, maugomvi, mavurugu, chumi zimeshuka, huko hawafanyi vizuri kama tunavyofanya sisi.
“Ulaya na Marekani sasa hivi hawafanyi vizuri kiuchumi kama tunavyofanya sisi huku, hata ndani ya kanda yetu hii ya Afrika Mashariki, Tanzania tunafanya vizuri”.Amesema Rais Samia.