pmbet

Ureno na Uhispania hapatoshi leo fainali UEFA Nations League

Sisti Herman

June 8, 2025
Share :

Wapinzani wa kandanda wa Iberia, Ureno na Uhispania watacheza hatua ya fainali ya UEFA Nations League 2025 leo saa 4 usiku kwenye Uwanja wa Allianz Arena mjini Munich, Ujerumani.

 



Utakuwa usiku wa kihistoria bila kujali matokeo, kwani timu zote zinawania kuwa mabingwa mara mbili wa UEFA Nations League. Ureno ilishinda toleo la kwanza mnamo 2019 wakati Uhispania ilitawazwa mabingwa mnamo 2023.

Fainali pia itashuhudia simulizi ya kuvutia - Cristiano Ronaldo akiwakilisha Ureno dhidi ya Mhispania mwenye umri wa miaka 17 Lamine Yamal, chipukizi wa soka duniani.

Ureno ilitinga fainali baada ya kuwalaza wenyeji Ujerumani mabao 2-1 katika nusu fainali ya kwanza Jumatano. Ronaldo alifunga bao la ushindi - bao lake la 137 kwa Ureno - na kuimarisha zaidi nafasi yake kama mfungaji bora wa muda wote katika soka ya kimataifa.

Uhispania ilijikatia tiketi ya fainali kwa ushindi wa 5-4 dhidi ya Ufaransa mjini Stuttgart siku ya Alhamisi. Yamal alifunga mabao mawili kwa msisimko wa mabao tisa na kuongeza umaarufu wake kama nyota gwiji.

Uhispania ya Luis de la Fuente inaingia kwenye mpambano wa taji bila kushindwa katika mechi 10 zilizopita za ugenini.

Ureno, chini ya Roberto Martínez, wamepoteza mchezo mmoja tu kati ya tisa zilizopita kwenye shindano hilo.

Uhispania wanashikilia faida kubwa dhidi ya Ureno katika rekodi za kukutana wao kwa wao, Uhispania wameshinda 18 kutoka kwa mechi 40. Ureno wameshinda mara sita huku mechi 16 zikimalizika kwa sare.

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet