Yanga kucheza na Rayon Sports June 15
Sisti Herman
June 1, 2025
Share :
Klabu ya Yanga SC ya Tanzania inatarajia kucheza mechi ya Kimataifa ya kirafiki dhidi ya Rayon Sports Juni 15, 2025 mchezo huo ukiwa unalenga kujenga uhusiano mzuri na klabu hiyo.
Mchezo huo utachezwa Mjini Kigali, Rwanda.
Kukubali mwaliko huo kwa Yanga kunathibitisha dhamira yao ya kukataa kucheza mechi dhidi ya watani wao Simba mechi iliyoahirishwa Machi 8, 2025.