pmbet

Yanga wafanya kikao na Tarura kuhusu ujenzi wa uwanja.

Joyce Shedrack

March 11, 2026
Share :

Uongozi wa klabu ya Yanga chini ya Rais wake Hersi Said, leo umefanya kikao cha pili na Ofisi za TARURA pamoja na wadau mbalimbali kujadili maendeleo ya mradi wa ujenzi wa uwanja wa klabu hiyo.

Kikao hicho kimekuja kufuatia ukaguzi uliofanywa katika eneo lililotengwa kwa ajili ya mradi huo, ambapo katika mkutano wa leo kulifanyika uwasilishaji wa ramani pamoja na maelezo ya kina kuhusu uwanja unaotarajiwa kujengwa.

Wadau waliohudhuria kikao hicho walipata nafasi ya kujadiliana mambo mbalimbali muhimu yanayohusu utekelezaji wa mradi huo.
 

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet