Yona Amos kwenye mawindo ya Simba.
Joyce Shedrack
December 26, 2025
Share :
Klabu ya Simba inaripotiwa kuaangalia uwezekano wa kunasa saini ya golikipa wa Pamba JIJI Yona Amos wakati wa dirisha dogo la usajili ili kuchukua nafasi ya mlinda mlango Yakoub Suleiman ambaye amepata majeraha akiwa na timu ya Taifa.

Simba wanalazimika kusajili golikipa mwingine kutokana na magolikipa wote wawili kupata majeraha ambayo yatawaweka nje ya uwanja muda ambao timu itakuwa na michezo ya muhimu.





